Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 54 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 442 2017-06-23

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI (K.n.y MHE. ESTHER L. MIDIMU) aliuliza:-
Barabara za Vijiji katika Wilaya ya Maswa ni mbovu kiasi kwamba sehemu nyingi za maeneo ya vijijini hayapitiki.
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha za kutosha za Mfuko wa Barabara ili barabara hizo zifanyiwe matengenezo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Maswa inao mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 1,055. Kwa mwaka wa fedha 2017/2018, Halmashauri hiyo imetengewa shilingi bilioni 1.4 kutoka katika Mfuko wa Barabara kwa ajili ya kufanya matengenezo ya kawaida kilometa 203.5, matengenezo ya sehemu korofi kilometa 54, matengenezo ya muda maalum kilometa 32, kujenga madaraja manne, Makalvati yenye urefu wa mita 28 na mtandao wa kupitisha maji ya mvua yenye mifereji ya mita 400.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutafuta fedha ili kuimarisha mtandao wa barabara za Halmashauri hapa nchini.