Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 8 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 67 2016-04-29

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:-
Katika Jimbo la Korogwe Vijijini yako mashamba ambayo tangu yabinafsishwe hayajaendelezwa:-
(a) Je, ni lini mashamba hayo yatagawiwa kwa wananchi kwa sababu hayaendelezwi?
(b) Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuyatoa kwa wananchi mashamba ambayo hayaendelezwi ili kuwapa fursa ya kuyatumia kwa shughuli za kilimo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba nijibu swali namba 67 la Mheshimiwa Stephen Hilary Ngonyani, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Stephen Hilary Ngonyani, naomba kutoa maelezo ya utangulizi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeziagiza Halmashauri zote nchini kukagua mashamba na kuwasilisha taarifa za ukaguzi na hatua stahiki. Mashamba yatakayobainika kwamba hayajaendelezwa ilani ya ubatilisho zitatumwa na Wakurugenzi husika kwa umilikishaji. Baada ya kipindi cha siku 90 kumalizika Halmshauri zitatakiwa kuleta mapendekezo ya ubatilisho Wizarani.
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, ukaguzi uliofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, umebaini kuwepo kwa shamba lisiloendelezwa la Mwakijubi Farm linalomilikiwa na Ndugu Chavda. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ameanza kufanya taratibu za ubatilisho wa milki kabla ya kuwasilisha mapendekezo Wizarani.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, ugawaji wa mashamba kwa wananchi hufanyika baada ya taratibu za ubatilisho kukamilika na kupata kibali cha Mheshimiwa Rais. Taratibu za ubatilisho zinapokamilika mashamba haya hurejeshwa katika Halmashauri husika ili yapangiwe matumizi mengine ikiwemo kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni rai yetu sasa baada ya taratibu za ubatilisho kukamilika na maeneo haya kukabidhiwa kwenye Halmashauri, Halmashauri watapanga matumizi kulingana na uhitaji wa eneo husika ikiwa ni pamoja na matumizi ya kilimo. Kwa sasa, wakati zoezi la ubatilisho linafanyiwa kazi, tunaomba wananchi waendelee kuvuta subira mpaka hapo mchakato wa ubatilisho utakapokamilika.