Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 399 2017-06-16

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:-
Katika Jimbo la Segerea zipo shule kumi na moja za sekondari za Serikali ambapo wanafunzi wa shule hizo wanafaulu vizuri kwa kupata daraja la I, II na III na kuwa na sifa ya kujiunga kidato cha tano. Kwa mfano mwaka 2015 wanafunzi zaidi ya 400 walifaulu kwenda kidato cha tano, lakini katika Jimbo la Segerea hakuna hata shule moja ya kidato cha tano licha ya kuwa na maeneo ya kujenga ya kutosha katika shule za sekondari za Kinyerezi, Magoza na Ilala.
Je, Serikali ina mpango gani madhubuti wa kuanzisha shule za kidato cha tano na sita katika maeneo ya shule zilizotajwa ili kuwapunguzia wanafunzi hao adha ya usafiri wanayopata kwa kufuata shule mbali?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ina jumla ya shule za sekondari za Serikali 49 zikiwemo shule sita kongwe. Kati ya shule hizo, saba ni za kidato cha tano na sita. Halmashauri inaendelea kuboresha miundombinu ya shule ya sekondari Juhudi ili iwe na Kidato cha tano na sita. Aidha, katika mpango wa muda mrefu Halmashauri imepanga kuanzisha shule sita za kidato cha tano na sita kuanzia mwaka 2017 hadi 2022. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha shule hizo zinakuwepo katika kila tarafa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za kidato cha tano na sita ni za kitaifa ambapo zinachukua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini, ndiyo maana wanafunzi 400 kutoka Jimbo la Segerea wamechaguliwa kwenda shule mbalimbali nchini.