Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 46 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 380 2017-06-13

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:-
Mhimili wa Mahakama kama ilivyo mihimili mingine unahitaji kuwa na eneo la uhakika la kufanyia kazi na vitendea kazi vya uhakika:-
(a) Je, ni lini Wilaya ya Korogwe itajengewa Mahakama ya Wilaya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU - K.n.y WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Pius Chatanda, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa Mahakama kama Mihimili mingine, wanahitaji mazingira mazuri na muafaka kwa kufanyia kazi zao. Aidha, napenda kukiri kuwa moja ya changamoto kubwa inayozikabili Mahakama zetu ni pamoja na uhaba wa majengo na uchakavu wa miundombinu iliyopo.
Mheshimiwa Spika, Mpango wa maendeleo wa ujenzi wa Mahakama kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ni pamoja na ujenzi wa Mahakama za Mkoa ikiwemo ujenzi wa Mahakama sita za Hakimu Mkazi, ujenzi wa Mahakama 15 za Wilaya na Ujenzi wa Mahakama 10 za Mwanzo.
Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Mahakama imepanga kujenga Mahakama ya Wilaya ya Korogwe kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Aidha, katika Mkoa wa Tanga Wilaya zilizopewa kipaumbele katika ujenzi ni Kilindi, Korogwe na Mkinga. (Makofi)