Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 46 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 378 2017-06-13

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA) aliuliza:-
Baadhi ya vituo vya Polisi na Magereza nchini vina majengo chakavu sana vikiwemo Kituo cha Polisi Bagamoyo na Gereza la Kigongoni Bagamoyo:-
Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kujenga nyumba za Polisi na Askari Magereza Bagamoyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli baadhi ya Vituo vya Polisi na Magereza nchini vina majengo chakavu ambayo yalijengwa miaka mingi iliyopita na kituo cha Polisi na Magereza Bagamoyo kikiwa miongoni mwao.
Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kujenga Kituo cha Polisi, Gereza na nyumba za kuishi za Askari katika Wilaya ya Bagamoyo na Wilaya nyingine nchini zisizo na majengo hayo, ujenzi huo utajengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha za bajeti. Sambamba na hilo, Wizara imeweka msisitizo katika matumizi ya rasilimali zilizopo kama vile ardhi ili kupunguza tatizo hili kwa kujenga vituo vya Polisi katika Wilaya 25 na Magereza katika Wialaya 52 kote nchini.