Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 366 2017-06-12

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA aliuliza:-
Kwa zaidi ya miaka kumi sasa Serikali imejenga jengo la ghorofa moja kwa ajili ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga lakini jengo hilo bado halijakamilika, ujenzi umesimama kwa muda mrefu hali inayosababisha jengo hilo kuharibika na kuanza kupoteza ubora wake. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sixtus Raphael Mapunda, Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi ya Wilaya ya Mbinga, Serikali imetenga shilingi milioni 250 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018. Fedha hizo zitatumika kukamilika ujenzi wa tanki la maji, uwekaji wa mfumo wa maji safi na maji taka, ujenzi wa uzio, ufungaji wa mfumo wa umeme,vifaa vya kuzuia moto, upigaji rangi na kukamilisha kazi ya nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuwasihi kwamba fedha hii itakapotolewa wahakikishe jengo hili linakamilika na kuanza kutumika mara moja.