Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 365 2017-06-12

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:-
Mkandarasi anayejenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino anaidai Serikali shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kukamilisha jengo la Halmashauri.
Je, ni lini Serikali itamlipa mkandarasi huyo kiasi hicho cha fedha ili ujenzi huo uweze kukamilika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Aloyce Bura, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya Mkandarasi aliyejenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, mpaka sasa ni shilingi milioni 758.2 yakiwemo madai yaliyohakikiwa ya shilingi milioni 368.0 na madai ambayo hayajahakikiwa ya shilingi milioni 390.2 ambayo yanaendelea kufanyiwa kazi. Katika mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri hiyo imepokea shilingi milioni 700 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi. Vilevile katika mwaka wa fedha 2017/ 2018 Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya kazi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizi zinapaswa zitumike kulipa deni ambalo Mkandarasi anadai kabla ya kuendelea na kazi nyingine. Serikali itaendelea kutenga fedha kila mwaka ili kuhakikisha ujenzi wa jengo hilo la Halmashauri unakamilika.