Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 360 2017-06-08

Name

Maida Hamad Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaamua kurudisha fedha zilizokusanywa na Halmashauri kupitia vyanzo vyake vya ndani ili ziweze kutekeleza majukumu yake na mikakati iliyopangwa kwa ufanisi?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maida Hamad Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Serikali za Mitaa zinakusanya mapato kupitia vyanzo vyake vya ndani kwa mujibu wa Sheria na Fedha za Serikali za Mitaa, Sura ya 290, kifungu cha 6, 7, 8 na 9. Ukusanyaji wa mapato hayo unasimamiwa na Sheria Ndogo zinazofafanua sheria mbalimbali za kodi zinazopaswa kukusanywa na mamlaka hizo.
Mheshimiwa Spika, mapato ya ndani yanayokusanywa na Halmashauri hutumika kwa shughuli za maendeleo na uendeshaji wa Halmashauri kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa na Halmashauri zenyewe kwa kuainishwa katika mipango na bajeti zao za kila mwaka. Jukumu la Serikali Kuu ni kuidhinisha mapato na matumizi ya fedha hizo, kusimamia na kudhibiti matumizi ili kuhakikisha yanazingatia sheria na taratibu za fedha zilizowekwa na kuhakikisha zinatumika kwa madhumuni ya kuwaletea maendeleo wananchi katika maeneo yao.
Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kukusanya mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa na kuwasilisha Serikali Kuu na kisha kuzirejesha kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa haupo.