Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 43 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 356 2017-06-07

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. MHE. AMINA N. MAKILAGI) aliuliza:-
Je, nini mipango ya Serikali ya kumaliza tatizo kubwa la nyumba za askari hapa nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amina Nassoro Makilagi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna tatizo kubwa sana la nyumba za Askari za kuishi. Kwa kufahamu hilo Serikali imekuwa ikitenga bajeti ya ujenzi wa makazi ya Askari kwa awamu kulingana na uwezo uliopo. Aidha pamoja na kutenga fedha hizo Wizara yangu itajielekeza zaidi kutumia rasilimali zilizopo na teknolojia rahisi ya ujenzi wa nyumba ili kupunguza tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia ubia baina ya Serikali na sekta binafsi Jeshi la Polisi limefanikiwa kujenga nyumba 353 Kunduchi na Mikocheni, Dar es Salaam kwa ajili ya askari wa kawaida na maafisa. Aidha, Jeshi la Magereza linaendelea na ujenzi wa nyumba 320 Ukonga, Dar es Salaam kwa fedha za Serikali na lipo katika mazungumzo ya ubia na Shirika la Nyumba la Taifa utakaowawezesha kujenga nyumba 100 Msalato, Dodoma. Kadhalika, Idara ya Uhamiaji inafanya makubaliano na Shirika la Nyumba la Taifa kwa ajili ya ununuzi wa nyumba 103 Dodoma, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la kuhamia Dodoma. Utaratibu huu utaendelezwa katika Mikoa mingine ili kupunguza changamoto hii kwa Askari wetu. (Makofi)