Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 42 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 346 2017-06-06

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza
(a) Je, kuna wachezaji wangapi wa nje wanaoruhusiwa kucheza kwenye Ligi Kuu Tanzania?
(b) Je, tulianza na wachezaji wangapi miaka ya nyuma na sasa wako wangapi?
(c) Je, ni zipi sababu za kuongeza au kupunguza wachezaji na ni nini manufaa yake?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venance Methusalah Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, lenye vipengele (a), (b) na (c), kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa taratibu za usajili za TTF wachezaji wa nje wanaoruhusiwa kucheza kwenye Ligi Kuu Tanzania ni saba kwa kila klabu. Tulianza na wachezaji watano kati ya mwaka 2010 hadi 2015 na baadaye kuanzia msimu wa 2015/2016 idadi imeongezeka na kufikia wachezaji saba.
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu ya kuongeza wachezaji wa nje kwenye Ligi Kuu hii ya Tanzania ni maombi ya wadau wenyewe wa mpira wa miguu, vikiwemo vilabu vya mpira wa miguu na mazingira mazuri ya mpira wa kulipwa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa wachezaji wa nje kwenye ligi kuu ya Tanzania umeongeza ushindani miongoni mwa wachezaji wetu kiweledi na kinidhamu na kuwa chachu ya vilabu kupanua wigo wao wa mapato kwa ajili ya usajili. Aidha, kuchanganya wachezaji wazawa na wageni ni fursa kwa wachezaji wetu kujifunza kutoka kwa wenzao na kunatangaza ligi yetu nje ya nchi ambako wachezaji wa kigeni wanatoka na maendeleo yao yanafuatiliwa kwa karibu na timu zao za Taifa.