Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2018-02-09

Name

Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AZZA H. HAMAD aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapelaka fedha za kutosha kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Shinyanga ambao umeanzishwa kwa nguvu za wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Azza Hillal Hamad, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kupitia fedha za ruzuku kutoka Serikalini imekamilisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD), nyumba moja ya mtumishi pamoja na jengo la kutolea huduma za ushauri nasaha ambalo liko katika hatua ya upauaji. Jumla ya shilingi milioni 365 zilitumika kutoka katika vyanzo mbalimbali kwa mchanganuo ufuatao:-
Ruzuku kutoka Serikali Kuu shilingi milioni 267; mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya shilingi milioni 86; nguvu za wananchi shilingi milioni saba na mchango wa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu shilingi milioni tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 zimetengwa shilingi milioni 110 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa hospitali hiyo ambapo kati ya hizo shilingi milioni 40 ni mapato ya ndani ya Halmashauri na shilingi milioni 70 ni ruzuku kutoka Serikali kuu. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2018/2019 zitatengwa shilingi milioni 110 kwa ajili ya kendeleza ujenzi wa hospitali hiyo ambapo shilingi milioni 50 ni mapato ya ndani ya Halmashauri na shilingi milioni 60 ni ruzuku kutoka Serikali Kuu. Serikali itaendeleza ujenzi wa hospitali hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha ili wananchi waweze kupata huduma.