Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 73 2018-02-06

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:-
Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:-
(a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala?
(b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Allan Joseph Kiula, Mbunge wa Iramba Mashariki, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miradi ya REA II haikukamilika katika Mkoa wa Singida ikiwemo Wilaya ya Mkalama baada ya Mkandarasi aliyekuwa akitekeleza miradi hiyo kampuni ya Spencon Services kushindwa kukamilisha kazi hiyo kama ilivyopangwa. Utekelezaji wa miradi hiyo ulifikia asilimia 65.
Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya Kampuni hiyo kushindwa kukamilisha kazi kwa asilimia 35 iliyobaki, vifaa kwa ajili ya kazi hizo vimehifadhiwa katika Ofisi ya TANESCO Mkoani Singida. Vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa Mkandarasi aliyepewa kazi hiyo Mwezi Januari, 2018. Kazi za miradi zilizobaki zinatarajiwa kukamilika ifikapo Mwezi Agosti, 2018
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkandarasi anayetekeleza miradi ya REA III Awamu ya kwanza katika Mkoa wa Singida ni Kampuni ya CCCE-ETERN-HEI Consortium ambapo mkataba wa kazi hiyo umesainiwa Mwezi Oktoba, 2017. Kazi za miradi zilianza Mwezi Oktoba, 2017 ambapo Mkandarasi amekamilisha kazi za upimaji na usanifu wa njia za kusambaza umeme pamoja na ununuzi wa vifaa. Mzunguko wa kwanza wa mradi huu Mkoani Singida unatarajwa kukamilika ifikapo Mwezi Juni, 2019, gharama ya mradi ni shilingi bilioni 41.5 wateja zaidi ya 2,997 wanatarajiwa kuunganishiwa umeme kupitia mradi huu.