Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 5 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 60 2018-02-05

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA aliuliza:-
Majengo ya Kituo Afya cha Kambi ya Jeshi Migombani Unguja ni chakavu na pia ni siku nyingi sana.
Je, ni lini Serikali itajenga kituo hicho ili kiwe cha kisasa na kiendane na wakati?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANO YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi wa Jeshi la Kujenga Taifa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Jeshi cha Migombani Zanzibar ni moja ya vituo vya tiba ambavyo huanzishwa katika kila Kikosi cha JWTZ ili kutoa huduma ya mwanzo ya tiba kwa Wanajeshi na familia zao, watumishi wa umma ikiwa ni pamoja na wananchi wanaishi jirani kabla ya kupelekwa katika hospitali za rufaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni, kweli majengo ya kituo hicho na vituo vingine vya JWTZ yamechakaa na kwa sababu ni ya muda mrefu. Kutokana na uchakavu huo wa Kituo cha Kambi ya Migombani na sehemu nyingine, ni matazamio ya Wizara kuvi karabati upya vituo vyote katika mwaka wa fedha 2018/2019 kadri hali ya upatikanaji wa fedha itakavyoruhusu.