Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2018-02-02

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Je, kuvunjwa kwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kuna faida gani kwa wakazi wa Dodoma?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini, maarufu kama mashine ya Kusini, kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilivunja Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) tarehe 15 Mei, 2017 kutokana na muingiliano wa kimamlaka kati yake na Manispaa ya Dodoma ambapo licha ya kuongeza gharama za uendeshaji, ulisababisha migogoro mingi ya kiuendeshaji, ikiwemo vyanzo vya mapato na migogoro ya ardhi, hali iliyosababisha kupungua kwa kasi ya maendeleo ya mji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuvunjwa CDA wananchi wamepata faida nyingi ikiwa ni pamoja na kupungua kwa gharama za uendeshaji ambazo zilibebwa na wananchi kupitia kodi, kuongezeka kwa kasi ya utekelezaji wa kazi, kuongezeka kwa mapato ya Halmashauri ambayo matumizi yake huamuliwa na Wawakilishi wa wananchi (Madiwani), kuongezeka kwa idadi ya watumishi, majengo, maabara na vitendea kazi vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko hilo limewezesha kuongeza ufanisi wa Manispaa katika kuwahudumia wananchi.
Aidha, ubadilishaji wa mikataba ya upangishaji (Ground Lease Agreements) za miaka 33 iliyokuwa ikitolewa na CDA kwa kuwapatia wananchi Hatimiliki za miaka 99 umehamasisha uwekezaji katika kuendeleza kwa kasi zaidi Mji wa Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi kifupi cha kuanzia Mei hadi Desemba, 2017 wananchi wamebadilisha jumla ya mikataba 19,000 kati ya 65,000 iliyotolewa na CDA kuwa kwenye mfumo mpya wa Hatimiliki za miaka 99.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na faida hizo, Manispaa ya Dodoma inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo madeni na migogoro iliyorithiwa kutoka CDA. Manispaa inakabiliana na changamoto hizo kwa kuimarisha makusanyo na kuimarisha usimamizi katika sekta ya ardhi.