Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 28 2018-01-31

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-
Tatizo la kupotea kwa watoto katika Jiji la Dar es Salaam limekuwa kubwa. Aidha, taarifa za kupotea kwa watoto hao zimekuwa zikitolewa kwenye vyombo vya habari:-
(a) Je, ni sababu zipi zinazochangia kuongezeka kwa tatizo hilo siku hadi siku?
(b) Je, kwa nini taarifa za upatikanaji wa watoto hao hazitolewi kwenye vyombo vya habari?
(c) Je, Serikali ina mkakati gani kuondoa tatizo hilo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri ya Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la upoteaji wa watoto katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Jiji la Dar es Salaam. Aidha, sababu za upotevu wa watoto hawa ni pamoja na uangalifu hafifu wa watoto kutoka kwa wazazi au walezi na jamii kwa ujumla, mazingira magumu wanayoishi baadhi ya watoto, imani za kishirikina, visasi kati ya familia na kupotea kwa bahati mbaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hali hiyo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kudhibiti matukio hayo kwa kutoa elimu kupitia programu ya Polisi Jamii kwa watoto mashuleni na wazazi kupitia mihadhara ya kijamii na vyombo vya habari. Jitihada hizo zimekuwa zikizaa matunda kwa kuongeza elimu ya usalama wetu kwanza miongoni mwa jamii na hivyo kuongeza umakini wa kulinda watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Disemba, 2017 kwa Mkoa wa Dar es Salaam walipotea watoto 184, ambapo watoto waliopatikana ni 176 na watoto ambao wanaendelea kutafutwa ni nane. Jeshi la Polisi linaendelea kutoa rai kwa taasisi na idara mbalimbali kama Ustawi wa Jamii kushirikiana na kuwa na programu za pamoja ili kutoa elimu ya kumlinda mtoto wa Tanzania.