Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 09 2018-01-30

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:-
Kasi ya usambazaji umeme vijijini ni kubwa, lakini katika baadhi ya maeneo, miundombinu inayotumika hasa nguzo hairidhishi.
Je, Serikali inaweza kutuambia ni viwango gani (standards) vinavyotumika katika utafutaji wa nguzo hizo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa miradi ya usambazaji umeme vijijini, Serikali imekuwa ikihimiza na kuzingatia ubora wa vifaa vinavyotumika hasa nguzo. Nguzo zinazotumika kwenye miradi hiyo hununuliwa kutoka viwanda mbalimbali vya hapa nchini na awali baadhi zilikuwa zinatoka nje ya nchi.
Wakati wa ununuzi Shirika la Umeme nchini TANESCO hutoa viwango vya ubora wa nguzo kwa viwanda vinavyohitajika na vinavyozingatia viwango vya kimataifa. Kwa kuzingatia viwango hivyo, nguzo kwa ajili ya usambazaji na usafirishaji wa umeme zinatakiwa kuwa na urefu kati ya mita tisa hadi 18 na kipenyo kati ya milimita 130 hadi 308.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazalishaji hutumia dawa bora kuzalisha nguzo hizo na TANESCO hufanya ukaguzi kabla ya kuanza kutumika ili kujiridhisha katika ubora wake.