Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 10 | Sitting 1 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu | 01 | 2018-01-30 |
Name
Hassanali Mohamedali Ibrahim
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kiembesamaki
Primary Question
MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. IBRAHIM MOHAMEDALI RAZA) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itachukua hatua kwa kuwasaidia vijana walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya?
Name
Antony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ibrahim Mohamedali Raza, Mbunge wa Kiembe Samaki kama ifutavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua tatizo la matumizi ya madawa ya kulevya na athari yake kubwa kwa nguvu kazi ya Taifa letu ambayo asilimia kubwa ni vijana. Katika kukabiliana na tatizo hili, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imechukua hatua kadhaa kuwasaidia
vijana na makundi mengine walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya. Hatua hizo ni pamoja na zifuatazo:-
(i) Kutoa tiba kwa waathirika ambapo hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2017 jumla ya vituo vitno vya tiba (methadone) kwa waathirika wa dawa za kulevya vilikuwa vimeanzishwa nchini katika Hospitali za Muhimbili, Temeke, Mwananyamala, Zanzibar na Mbeya. Kupitia vituo hivyo, jumla ya waraibu 5,830 walipatiwa tiba na wengine wanaendelea kupatiwa matibabu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, mwaka huu wa 2018, Serikali inatarajia kufungua vituo vipya vya tiba katika Mikoa ya Mwanza na Dodoma. Kutokana na utafiti uliofanywa mwaka 2014, Serikali imepanga kufungua vituo vya tiba katika Mikoa ya Pwani, Morogoro, Arusha, Kilimanjaro na Tanga kwa kulingana na upatikanaji wa fedha.
(ii) Kuanzisha kituo kikubwa cha kuwapatia waathirika tiba kwa njia ya kazi (occupational therapy) ambapo mafunzo ya stadi za kazi mbalimbali yatatolewa. Kituo hiki kinajengwa katika eneo la Itega, Mkoani Dodoma.
(iii) Serikali kwa kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, imetengeneza miongozo mbalimbali kwa ajili ya kusimamia utoaji wa huduma kwa waathirika wa dawa za kulevya kuanzia katika vituo vya afya hadi kwenye huduma za kijamii zinazotolewa na asasi mbalimbali za kiraia.
(iv) Kutoa elimu kwa njia ya redio na luninga ambapo viongozi wa ngazi tofauti wa mamlaka wamekuwa wakitoa elimu katika vipindi mbalimbali. Vilevile elimu imekuwa ikitolewa katika shughuli za Kitaifa kama vile Mwenge, Nane Nane, maadhimisho na matamasha mbalimbali.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved