Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 115 2017-11-17

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:-
Vijiji 17 pekee kati ya vijiji 64 ndivyo vilivyopata umeme katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki na ni vijiji saba tu vya Ludewa, Mtego wa Simba, Kidugaro, Lung’ala, Mangala na Kinonko vilivyo katika orodha ya kupatiwa umeme katika REA III awamu ya kwanza ya mwaka 2017/2018.
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 47 vilivyosalia?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa vijiji 17 kati ya vijiji 64 ndio vilipatiwa umeme katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki. Vijiji vingine saba vitapatiwa umeme katika mzunguko wa kwanza wa mpango wa tatu wa REA ulioanza hivi karibuni. Kampuni ya State Grid ya Tanzania ambayo ndio mkandarasi wa eneo hilo tayari ameshaanza kazi katika vijiji hivyo saba ambavyo tumeviongeza. Katika eneo hilo kazi inajumuisha ujenzi wa njia ya kilometa 16.5 ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 pamoja na kilometa 16 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4. Kazi nyingine ni ufungaji wa transformer nane pamoja na kuunganisha wateja 256. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 1.2 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2019.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vingine vilivyobaki vitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili wa REA Awamu ya Tatu unaoendelea ambapo kwa pamoja utakamilika mwezi Julai, 2019 baada ya mzunguko kukamilika. Mradi huu utakamilika, kama nilivyosema mwaka 2020/2021.