Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2017-11-17

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-
Tatizo la uhaba wa watumishi wa Idara ya Afya Urambo linaathiri utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.
(a) Je, Serikali inachukua hatua gani za dharura katika kuliondoa tatizo la uhaba wa watumishi wa Idara ya Afya Wilayani Urambo?
(b) Je, Serikali inaweza kuchukua vijana wa Urambo na kuwapeleka vyuoni kusoma kwa makubaliano ya kurudi kufanya kazi Urambo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE)alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ina upungufu wa watumishi wa kada ya afya. Tatizo hili linazikabili Halmashauri nyingi nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa na utaratibu wa kuwaajiri wataalam wa kada ya afya kipindi wanapohitimu mafunzo na kufaulu vizuri katika masomo yao. Aidha, kuanzia mwezi Novemba, 2015 Serikali ilisitisha zoezi la kuajiri ili kubaini watumishi wa umma walioajiriwa na hawakuwa na sifa stahiki na kuwatambua watumishi halali.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukamilisha zoezi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeendelea kutoa vibali vya watumishi wa kada za afya ambapo mwezi Aprili, 2017 tulipata kibali cha kuajiri madakrati 209. Katika kibali hicho, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ilipata madaktari wawili. Vilevile mwezi Julai, 2017 tumepokea kibali cha watumsihi 2,152 ambao wamepangiwa katika Mikao na Halmashauri kwa uwiano ili kupunguza uhaba wa watumishi. Katika mgao huu Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ilipata watumishi 17. Serikali itaendelea kupanga watumishi kwa kadri bajeti itakavyokuwa inaruhusu
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa kuwasomesha vijana kwa makubaliano ya kurudi kufanyakazi umeshindwa kufanikiwa kwani uzoefu unaonesha vijana wengi wamesomeshwa na kuhitimu wanakuwa wamebadili mawazo na kuamua kufanyakazi sehemu nyingine na kuacha mgogoro kati ya wasomeshaji na aliyesomeshwa. Serikali inaendelea kuboresha mazingira kama vile upatikanaji wa nyumba pamoja na huduma za kijamii ili kuwafanya watumishi wanaoajiriwa waweze kubakia katika maeneo waliyopangwa.