Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 97 2017-11-16

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:-
Serikali iliipatia Halmashauri ya Wilaya ya Magu fedha za ujenzi wa ofisi za halmashauri, lakini ujenzi huo haujakamilika:-
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga Boniventura Desdery, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, awamu ya kwanza ya ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Magu ilianza tarehe 12 Januari, 2013 kwa kutumia Mkandarasi Beijing Construction Engineering Group wa Dar-es-Salaam. Ujenzi wa Jengo hilo unatarajia kugharimu jumla ya Sh.6,765,596,533.05 hadi kukamilika kulingana na usanifu uliofanyika. Kati ya fedha hizo Sh.2,744,537,216.94 zimeshapokelewa na kutumika tangu mwaka 2013 ujenzi ulipoanza.
Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2017/ 2018, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 600 kuendelea na ujenzi. Katika robo ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2017/ 2018 Serikali imetoa jumla ya shilingi milioni 200 ambazo zimepokelewa na halmashauri na mkandarasi anaendelea na ujenzi katika jengo hilo la halmashauri yake.