Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 9 | Sitting 6 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 77 | 2017-11-14 |
Name
Bupe Nelson Mwakang'ata
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:-
Serikali ilipanga kujenga na kupanua Uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini:-
Je, ni lini ujenzi huo utakamilika pamoja na kuwalipa fidia wananchi wanaozunguka uwanja huo?
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa ukarabati wa uwanja wa ndege wa Sumbawanga upo kwenye hatua ya manunuzi. Mkataba wa usimamizi wa kazi ya ujenzi ulitiwa saini baina ya Serikali na kampuni ya SMEC kutoka Australia mwezi Oktoba, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Mwezi Juni, 2017 Serikali ilitiliana saini mkataba wa ujenzi wa ukarabati wa uwanja huo na Kampuni ya Sino-Shine Overseas Construction and Investment East Africa Limited kutoka Nchini China. Utekelezaji wa mradi huo utakapoanza unategemewa kukamilika ndani ya miezi 18. Kazi ya ujenzi wa uwanja huo zitaanza mara baada ya Serikali kukamilisha taratibu za malipo ya fidia kwa wananchi wanaostahili kulipwa ili waondoke kupisha ujenzi wa uwanja.
Mheshimiwa Naibu Spika, maandalizi ya ulipaji wa fidia kwa wananchi watakaoathirika na mradi huo yapo katika hatua ya uhakiki wa mwisho kabla ya ulipaji wa fidia kuanza.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved