Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 9 | Sitting 6 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi | 76 | 2017-11-14 |
Name
Edward Franz Mwalongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Njombe Mjini
Primary Question
MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:-
Elimu ya ufundi ni muhimu ili kuwawezesha vijana kuajiriwa na kujiajiri:-
• Je, nchi yetu ina vyuo vingapi vya Ufundi Stadi vya Umma?
• Je, kuna vyuo vingapi visivyo vya Umma?
• Je, hivi vyote vina uwezo wa kudahili vijana wangapi kwa mwaka?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu kwa mwaka wa 2016/2017 ilikuwa na jumla ya vyuo vya ufundi stadi 127 vya umma na vyuo 634 visivyo vya umma vilivyokuwa vinatambulika na kusajiliwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA). Vyuo 501 kati ya 761 vilipata ithibati ya VETA na viliweza kudahili jumla ya wanafunzi 56,420 kwa mwaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Vyuo vya ufundi stadi vina umuhimu mkubwa wa kuandaa nguvukazi ya kutosha, mahiri na yenye ujuzi unaotakiwa ili iweze kushiriki katika kujenga uchumi wa viwanda wakati tunaelekea kwenye nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa 2016/2017 - 2020/2021 imelenga kuongeza idadi ya wahitimu katika vyuo vya ufundi stadi kutoka 150,000 kwa mwaka 2015 hadi kufikia 700,000 ifikapo mwaka 2021 ili kuongeza fursa za ajira kwa vijana wenye ujuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itakamilisha ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi ngazi ya mkoa katika mikoa mitano na ngazi ya wilaya katika wilaya sita. Aidha, itakamilisha ukarabati wa vyuo vya ufundi stadi katika wilaya mbili. Mkakati uliopo ni Serikali kuendelea kutenga bajeti ya maendeleo kila mwaka pamoja na kutafuta wafadhili mbalimbali wa ndani na nje ya nchi ili kuweza kujenga vyuo vingine.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved