Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2017-11-14

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vifaa tiba kwenye Hospitali ya Wilaya ya Singida Mjini au kituo cha afya Sokoine?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sima, Mbunge kutoka Singida, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanikiwa kununua vifaa tiba vyenye thamani ya Sh.102,939,700.00 kwa kutumia fedha za Mfuko wa Afya wa Pamoja na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya. Vifaa vilivyonunuliwa ni vitanda vitatu
(a) vya kujifungulia, mitungi mitano (5) ya kuhifadhia gesi, vitanda ishirini (20) vya hospitali na mashine tatu (3) za kutakasia vyombo vya hospitali. Vifaa vingine vilivyonunuliwa ni pamoja na mashine moja (1) ya kutolea dawa ya usingizi (anaestheric machine), kitanda kimoja (1) cha upasuaji (operation table) na mashine ya kutakasia vifaa tiba vyenye ujazo wa lita 100.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, Serikali imetenga jumla ya Sh.160,866.466.01 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwenye kituo cha afya cha Sokoine. Kati ya fedha hizo, Sh.41,451,400 zimeshalipwa Bohari Kuu ya Dawa (MSD)kwa ajili ya vifaa tiba. (Makofi)