Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 5 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 63 2017-11-13

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:-
Mkoa wa Tabora umepata usafiri wa uhakika wa ndege ya ATCL na kwa kuwa Tabora ina historia mbalimbali na kumbukumbu za mambo ya kale.
Je, Serikali ipo tayari kuutangaza Mkoa wa Tabora kwa utalii?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwanne Ismail Mchemba, Mbunge wa viti maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tabora umo katika Kanda ya Kati inayounganisha Mikoa ya Dodoma, Singida na Kigoma. Ni kweli kabisa kuwa Mkoa wa Tabora kama sehemu ya Kanda ya Kati una historia mbalimbali na kumbukumbu za mambo ya kale ikiwa ni pamoja na Tembe lililokaliwa na missionary Dkt. Livingstone, ambaye ni mpinga biashara ya utumwa kutoka Uingereza mwaka 1871 akiwa njaini kuelekea Ujiji - Kigoma. Pia kuna kituo cha njia ya kati ya biashara ya utumwa na vipusa vilivypo Ulyankulu eneo la Mtemi Mirambo na Gofu lililokuwa hospitali ya kwanza ya Kijerumani katika Mkoa wa Tabora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tembe la Dkt. Livinstone limekarabatiwa na kuna Watumishi ambao wanatoa maekelezo kwa wageni wanaotembelea kituo hicho. Katika mwaka wa fedha 2013 hadi 2017 kituo kilitembelewa na wageni 1,642 na jumla ya shilingi 2,292,000 zilikusanywa kutoka kwa watalii wa ndani na nje. Aidha, mipango ya usimamizi wa maeneo mengine niliyoyataja hapo juu imeandaliwa ili yaendelezwe kuwa vituo vya kumbukumbu na taarifa kwa matumizi mbalimbali yakiwemo ya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufanisi wa utangazaji, utalii wa Mkoa wa Tabora juhudi za utangazaji zinahusu vivutio vingine zaidi ya vivutio vya mambo ya kale vinavyopatikana katika eneo hilo. Juhudi hizo zinahusu utamaduni, wanyamapori, mazao ya nyuki na historia pana ya harakati mbalimbali za kijamii za nchi yetu zilizofanyika Mkoani Tabora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa juhudi za kuendeleza na kuutangaza Mkoa wa Tabora kiutalii zimekuwa zikiendelea hata kabla ya kuwepo kwa usafiri wa ndege ya ATCL. Kwa kuwa sasa Mkoa umepata usafiri wa uhakika wa ndege ya ATCL, Serikali itaongeza juhudi za kuutangaza Mkoa wa Tabora nje na ndani ya nchi ili kuhakikisha wageni wengi wanatembelea Mkoa huo kwa lengo la kukuza utalii na kuongeza pato la Taifa.