Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 94 2017-11-15

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS NYIMBO aliuliza:-
Kuna taarifa zilizotolewa na Wizara ya Nishati na Madini za kugunduliwa kwa gesi ya Hellium yenye ujazo wa takribani futi bilioni 54 za ujazo nchini.
Je, Serikali imejiandaaje kimkakati kuhusu ugunduzi huo na uchimbaji wa gesi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa mataifa makubwa kama Marekani yalishatangaza kukosekana kwa gesi hiyo ifikapo 2030?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos Nyimbo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Kampuni ya Hellium One Ltd. imegundua kiasi cha gesi ya Hellium yenye ujazo wa cubic feet 54 billions katika maeneo ya Ziwa Rukwa. Ugunduzi huo ulitokana na uchunguzi wa sampuli tazo za Mavujia yaani gas seeps ya gesi ya Hellium katika maeneo hayo kiasi ambacho kinakadiriwa kuwa kikubwa zaidi ya mara sita ya mahitaji ya dunia kwa sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Hellium One Ltd. imegundua madini ya hellium kupitia Kampuni zake tanzu za Gogota Tanzania Ltd., Njozi Tanzania Ltd. na Stahamili Tanzania Ltd. zinazomiliki leseni z utafutaji wa gesi ya hellium katika Mkoa wa Rukwa ikiwemo maeneo ya Ziwa Rukwa. Kampuni hizi zilipewa leseni za utafutaji wa hellium katika maeneo mbalimbali kuanzia mwaka 2015. Shughuli za utafutaji wa kina wa gesi ya helium unaendelea kwa kukusanya taarifa zaidi za kijiolojia, kijiokemia, kijiofizikia na 2D Seismic Survey ili zitumike kwa ajili ya uchorongaji wa visima vya utafiti yaani exploratoty wells. Kazi ya uchorongaji ikikamilika itawezesha kuhakiki kiasi halisi cha gesi ya hellium kilichopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uchimbaji wa gesi ya hellium utaanza mara baada ya kazi ya utafiti wa kina, upembuzi yakinifu na tathmini ya athari za mazingira, kukamilika kwa leseni ya uchumbaji wa gesi hiyo kutolewa. Matokeo ya gesi hizo ndiyo yatakayoonyesha kama kiasi cha gesi kilichopo kinaweza kuchimbwa kibiashara kwa kipindi gani na taifa litanufaikaje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kufundisha wataalam stahiki yaani wajiolojia, wahandisi wa migodi na wachumi wa madini kusudi wawe na ujuzi wa kutosha na hadi sasa Serikali ina jumla ya wataalam 454 wenye fani za mafuta na gesi katika viwango mbalimbali na elimu. Pia kuna wanafunzi 137 walipo katika mafunzo ya mafuta na gesi katika ngazi za shahada za uzamivu katika vyuo mbalimbali nje ya nchi na wanafunzi 455 katika ngazi ya diploma na shahada ya kwanza ndani ya nchi.