Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2017-11-08

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MARWA R. CHAHA (K.n.y. MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:-
Akiwa katika Kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 Mheshimiwa Rais aliahidi ujenzi wa barabara ya lami (Kasulu Road) ili kufungua Mji wa Ujiji:-
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi huo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sabreena Hamza Sungura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania aliahidi ujenzi wa kilomita10 za barabara kwa kiwango cha lami ndani ya Manispaa ya Kigoma Ujiji. Kutokana na ahadi hiyo, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji imeamua kujenga barabara ya Ujiji
– Bulenga - Bangwe yenye urefu wa kilomita 7.5 ambapo usanifu umekamilika na itagharimu shilingi bilioni 11.6 ambapo ujenzi unaweza kuanza mwaka wa fedha 2018/2019 na barabara ya Ujiji hadi Daraja la Mngonya yenye urefu wa kilomita 2.5, hivyo kufanya jumla ya kilomita10 ambazo Mheshimiwa Rais aliahidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ili uunganishe na ile barabara ya kutoka Kasulu lazima upembuzi yakinifu na usanifu wa barabara hiyo ufanyike kuunganisha kutoka Daraja la Mungonya hadi barabara Kigoma - Kasulu katika eneo la Msimba lenye urefu wa kilomita tatu. Kipande hicho cha kutoka Daraja la Mngonya hadi Msimba hakijafanyiwa upembuzi yakinifu. Kwa hiyo, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma inashauriwa kuweka kipaumbele na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara kutoka Daraja la Mto Mngonya hadi Msimba kwa kiwango cha lami.