Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2017-11-08

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:-
Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Morogoro umekamilika lakini haina umeme wala maji:-
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme na maji katika hospitali hiyo ili ianze kutumika na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dokta Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya mifumo ya umeme na maji katika Hospitali mpya ya Wilaya ya Morogoro. Ifikapo tarehe 15 Novemba, 2017, Sh.25,240,969.33 zitakuwa zimelipwa kwa ajili ya kuingiza umeme hospitalini hapo. Hadi sasa TANESCO wameshaweka nguzo na mfumo wa umeme katika jengo la hospitali, kazi iliyobaki ni kufunga transfoma ili umeme uweze kuwashwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa miundombinu ya maji hospitalini hapo utakaogharimu shilingi milioni 50 unaendelea. Kati ya hizo, shilingi milioni 21 zimeshapelekwa kulipia kazi zinazoendelea. Mifumo ya huduma ya maji itakuwa imekamilika ifikapo mwishoni mwa Januari, 2018.