Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 295 2017-05-29

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Leseni ya utafiti wa uchimbaji wa dhahabu ya Mabangu imechukua muda mrefu sana katika Kata za Nyakafuru na Bukandwe.
Je, ni lini mgodi wa uchimbaji dhahabu baina ya Mabangu na Resolute utaanza uzalishaji?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mradi wa Nyakafuru (Nyakafuru Gold Mining Project) unahusisha leseni 22 za utafutaji wa Madini zinazomilikiwa na Kampuni ya Mabangu Mining Limited ambayo ni Kampuni tanzu ya Resolute Tanzania Limited. Mashapo (deposit) katika mradi huu yamesambaa katika leseni hizi ambazo maeneo yake yana ukubwa ya kilometa 1.4 hadi 25.17. Mashapo yaliyogunduliwa katika leseni hizi kwa pamoja ndiyo yanaweza kuchimbwa kibiashara. Hata hivyo kati ya leseni 22, leseni tisa kampuni imeamua kuziachia.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Kampuni ya Mabangu Limited ni Kampuni tanzu ya Resolute Tanzania Limited, na kwa kuwa Kampuni ya Resolute Tanzania Limited iliyokuwa inamilikiwa na Golden Pride ya Nzega inadaiwa kodi na TRA, Kampuni ya Mabangu sasa inahusishwa na deni hilo la shilingi bilioni 147.007. Kutokana na Kampuni hiyo kuhusishwa na deni hilo, anayetarajiwa sasa kuwa mbia wa Kampuni ya Manas Resources mwenye jukumu la kufadhili mgodi ameamua sasa kupeleka mbele ufadhali wake.
Mheshimiwa Spika, mpango wa mradi wa Nyakafuru sasa utaanza kuzalishaji dhahabu mwezi Juni, 2019 baada ya masuala ya kodi kukamilika na kupata leseni ya uchimbaji pamoja na mazingira.