Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 278 2017-05-26

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI aliuliza:-
Kumekuwa na tatizo kubwa la maji katika Wilaya ya Musoma Vijijini hasa vijiji vya Kabulabula, Bugoji, Kangetutya na Saragana. Aidha, visima vilivyochimbwa na wanakijiji hao vinakauka wakati wa kiangazi.
Je, ni lini Serikali itahakikisha programu za maji zinapelekwa na zinatekelezwa kwa umakini katika Wilaya ya Musoma Vijijini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joyce Bita Sokombi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli visima vingi hasa vilivyochimbwa na kufungiwa pampu hukauka wakati wa kiangazi na hivyo kuathiri upatikanaji wa huduma katika maeneo husika. Sababu kubwa ni mabadiliko ya tabianchi hali inayosababisha maji kupatikana katika kina kirefu zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua changamoto hiyo, Serikali kupitia Programu ya Uendelezaji wa Sekta ya Maji (WSDP II) imeanza kufanya usanifu wa mradi mpya utakaotumia Ziwa Victoria kama chanzo cha maji cha uhakika. Vijiji vitakavyoingizwa katika mpango huo ni Kabulabula, Bugoji na Saragana.