Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 5 Works, Transport and Communication Ofisi ya Rais TAMISEMI. 43 2016-04-25

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Mafuriko yanayotokea Mtwara Mjini kila mwaka hasa katika Kata ya Shangani, Cuono, Magomeni na Ufukoni yanasababishwa namiundombinu mibovu ambayo imejengwa chini ya kiwango katika maeneo mengi ya Mji wa Mtwara:-
(a) Je, Serikali iko tayari sasa kujenga upya mitaro, madaraja pamoja na miundombinu mingine ili maji yaweze kusafiri kuelekea baharini wakati wa masika?
(b) Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya Mikindani - Lwelu ufukweni mwa bahari kwa kiwango cha lami ikizingatiwa kuwa barabara hiyo iko ndani ya Manispaa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2015/2016 imetenga Dola za Kimarekani 540,000 kupitia mradi wa Tanzania Strategic Cities Project (TSCP) kwa ajili ya upembuzi yakinifu, usanifu na ujenzi wa mradi wa barabara ambao utahusisha ujenzi wa mitaro na madaraja ambao utahusisha uboreshaji wa miundombinu iliyoharibika na mvua. Utekelezaji wake upo katika kukamilisha hadidu rejea ili utaratibu wa manunuzi ya kupata Mkandarasi Mshauri ziweze kufikika.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshaanza matengenezo ya barabara ya Mikindani- Mchuchu- Lwelu kwa kiwango cha lami, ambapo katika mwaka wa fedha 2013/14 kilometa moja ilitengenezwa kwa kiwango cha lami. Aidha, ili kuhakikisha barabara hiyo inapitika wakati wote, Serikali katika Bajeti ya mwaka 2016/2017 imetenga shilingi 89,000,000 kwa ajili ya kuifanyia matengenezo. Azma ya Serikali ni kuijenga barabara hiyo yote ya kilometa 11 zilizobaki kwa kiwango cha lami kadri upatikanaji wa fedha utakavyoruhusu.