Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 94 2017-09-13

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. MHANDISI ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Gereza la Wilaya ya Kibondo – Nyamisati limekuwa na ongezeko kubwa sana la wafungwa na mahabusu kwa sababu ya uwepo wa wakimbizi.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati unaofaa kupeleka mradi mkubwa wa maji kwenye gereza hilo ili kulinda afya za raia na askari walioko kwenye gereza hilo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Atashasta Nditiye, Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa kuna tatizo la upatikanaji wa maji katika Gereza la Kibondo. Mwaka 2010, Serikali kupitia Jeshi la Magereza lilitenga fedha kiasi cha shilingi milioni 20 kwa ajili ya kuchimba kisima kirefu na kazi hiyo ilifanywa na Wakala wa Uchimbaji Mabwawa na Visima iliyopo Ubungo Dar es Salaam. Uchimbaji wa kisima hicho ulikamilika tarehe 2 Oktoba 2010 na kilikuwa na uwezo wa kutoa lita 2,300 kwa saa ambayo ni sawa na lita 55,200 kwa siku. Kiasi hiki ni kidogo ukilinganisha na mahitaji halisi ya maji ya Gereza la Kibondo ambayo ni lita 94,870 kwa siku, hivyo kuwa na upungufu wa takriban lita 39,670 kwa siku.
Mheshimiwa Spika, mwaka 2014 upembuzi yakinifu ulifanywa na wataalam wa Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mhandisi wa Mamlaka ya Maji Wilaya ya Kibondo na kushauri kuwa ili gereza hilo liondokane na tatizo la maji, Jeshi la Magereza linapaswa kuvuta maji kutoka mtandao wa maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo hadi gerezani ambapo gharama zake ilikadiriwa kuwa ni shilingi 330,492,450. Hata hivyo, kutokana na ufinyu wa bajeti, mradi huo haujatekelezwa hadi sasa. Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha tatizo la maji Gereza la Kibondo linapata ufumbuzi wa kudumu.