Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 9 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 111 2017-09-15

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. SAADA MKUYA SALUM aliuliza:-
Vituo vya Afya vinavyomilikiwa na Jeshi la Wananchi vimekuwa vikitoa huduma za afya kwa wananchi wengi na kutokana na umadhubuti na umakini wa watendaji, wananchi wamejenga imani kubwa juu ya huduma zinazotolewa katika vituo hivyo; hata hivyo huduma hizo zimekuwa zikikabiliwa na vikwazo mbalimbali vikiwemo uhaba wa dawa, Madaktari na vitendea kazi:-
Je, Serikali imeweka mkakati gani madhubuti wa kuhakikisha kuwa vifaa tiba, dawa na Madaktari vinapatikana ili kutoa huduma bora?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saada Mkuya Salum, Mbunge wa Welezo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa linaendelea na hatua ya kuboresha huduma za tiba Jeshini, kama ifuatavyo:-
(a) Kuendeleza kuwashawishi wataalam wa tiba wenye sifa kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kulingana na nafasi za ajira zinazopatikana.
(b) JWTZ limeendelea na utaratibu wa kuwaendeleza Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma kupata elimu katika ngazi mbalimbali zikiwemo Stashahada, Shahada na Shahada ya Uzamili kupitia vyuo vyetu vya kijeshi mfano “Military College of Medical Services” pamoja na vyuo vya kiraia nje ya Jeshi. Aidha, Serikali kupitia Wizara ya Afya imeendelea kuwadhamini wataalam wa tiba wanaosomea Shahada ya Uzamili na Uzamivu.
(c) Serikali kupitia Wizara ya Afya imekuwa ikiendelea kutoa ruzuku na kuongeza upatikanaji wa madawa na vifaa tiba.
(d) Kupitia wafadhili mbalimbali mfano Serikali ya Marekani na Serikali ya Jamhuri ya Ujerumani, huduma za tiba zimeendelea kuboreshwa hasa kwa kuongeza miundombinu na vifaa tiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu niliyotoa katika sehemu (a) mpaka (d), Wizara yangu iko katika mchakato wa kuanzisha Mfuko wa Bima ya Afya kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. Ni imani yetu kuwa Mfuko huo utakapoanzishwa utaweza kuongeza rasilimali fedha katika utoaji huduma za afya Jeshini. Fedha hizo za ziada zitatumika katika kuboresha miundombinu na upatikanaji wa dawa na vifaatiba hivyo kuboresha huduma za afya kwa Wanajeshi na wananchi wanaotumia vituo vya afya vya Jeshi kupata tiba. (Makofi)