Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 73 2017-09-12

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:-
Jimbo la Ukonga lina shida kubwa ya umeme katika Kata zifuatazo; Kata ya Chanika (Ngwale, Nguvu Mpya, Virobo, Kidugalo, Yongwe, Lukooni, Vikongoro na Tungini); Kata ya Zingiziwa (Zogoali, Zingiziwa, Ngasa, Ngobedi, Somelo na Gogo, Lubakaya na Kimwani); Kata ya Majohe (KIvule na Viwege); Kata ya Buyuni (Zavala, Buyuni, Mgeule Juu, Nyeburu, Mgeule Chini, Kigezi, Kigezi Chini na Taliani); Kata ya Pugu Station (Bangulo, Pugu Station na Kichangani); Msongola (Yangeyange, Mbondole, Kidle, Mkera, Sangara, Kiboga, Uwanja wa Nyani, Kitonga, Mvuleni na Mvuti) na Kata ya Kivule (Bombambili). Maeneo hayo yote yanahudumiwa na Wilaya ya Kisarawe kama maeneo ya vijijini. Je, ni lini maeneo hayo yatapata umeme wa REA?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swai la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, maeneo ya Kidole, Bangulo, Kitonga, Mvuti na baadhi ya maeneo mengine pamoja na Msongole yalipatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Pili uliokamilika mwezi Disemba, 2016. Kazi ya kupeleka umeme katika maeneo hayo ilijumuisha pia vijiji vilivyokuwa vinatoka katika Wilaya ya Kisarawe ambapo pamoja na mambo mengine vimefungiwa transfoma 55 za kVA 50, kVA 100 na kVA 200; ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 pia umejengwa kwa urefu wa kilometa 187.22 lakini njia ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 239.7 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja 1,083. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 5.3.
Mheshimiwa Spika, mitaa mingine iliyobaki ya Kata za Chanika, Zingiziwa, Majohe, Buyuni, Pugu Station pamoja na Msongola, zitapatiwa umeme kupitia Mradi wa Urban Electrification chini ya ufadhili wa Maendeleo wa Benki ya Dunia.
Mheshimiwa Spika, kazi hizi zinajumuisha ujenzi wa njia ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 66.3, msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 336.7 pamoja na ufungaji wa transfoma 73 za kVA 200 na kVA 100. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 10.73 na utaunganishia wateja 7,083.