Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 6 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 71 2017-09-12

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Tatizo la makazi kwa wanajeshi wetu ni kubwa kiasi kwamba maaskari wetu kupata usumbufu na kuathiri utendaji kazi wao.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za makazi kwa wanajeshi wa upande wa Unguja?
(b) Je, ni nyumba ngapi Serikali imepanga kujenga Zanzibar?
(c) Je, ni lini ujenzi wa nyumba kwa upande wa Zanzibar utaanza?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Serikali inao mpango wa kuboresha makazi ya wanajeshi kwa kujenga nyumba za familia idadi ya 10,000. Kwa awamu ya kwanza ujenzi wa nyumba za familia za askari idadi 6,064 umefikia hatua ya mwisho kukamilika. Aidha, katika awamu hii hakuna ujenzi unaofanyika Unguja.
(b) Mheshimiwa Spika, katika awamu ya kwanza kwa upande wa Zanzibar, nyumba zimejengwa katika Kisiwa cha Pemba. Nyumba zilizojengwa ni ghorofa 40 zenye uwezo wa kuchukua familia idadi 320. Hatua inayofuata ni kukamilisha miundombinu ya umeme na maji ili nyumba hizo zianze kutumika.
(c) Mheshimiwa Spika, mchakato wa kuanza ujenzi wa nyumba za askari awamu ya pili unaotarajiwa kukamilisha ujenzi wa nyumba 10,000 unaendelea. Mgawanyo wa nyumba hizo utazingatia hitajio katika Kambi za Jeshi kwa ujumla ikihusisha Kambi za Unguja. Ujenzi huu utaanza mara mchakato utakapokamilika.