Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 47 2017-09-08

Name

Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBEDA H. SAKURU aliuliza:- Hivi sasa kumekuwa na wimbi la matukio ya ukamataji wa Wahamiaji haramu kwa wingi hapa nchini. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya ongezeko la matukio hayo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zubeda Hassan Sakuru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji imekuwa ikiendelea na mapambano dhidi ya wahamiaji haramu na kuwachukulia hatua za kisheria ili kuhakikisha nchi yetu inakuwa salama. Katika kupambana na wahamiaji haramu Idara ya Uhamiaji huchukua hatua zifuatazo:-
(i) Kuendesha doria za misako ya mara kwa mara katika maeneo mbalimbali nchini kwa kushirikiani na vyombo vya Ulinzi na Usalama ambapo katika mwaka 2016/2017 jumla ya watuhumiwa 9.581 na wahamiaji haramu walikamatwa na kuchukuliwa hatua mbalimbali kisheria.
(ii) Serikali inaendelea kuimarisha vitendea kazi kama vile magari na kupanua wigo wa watumishi ili kuweza kudhibiti mipaka mingi iliyopo na kutoa elimu kwa umma juu ya madhara ya kuhifadhi wahamiaji haramu na kupambana na mitandao wa wasafirishaji haramu wa binadamu.
Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali ni kuendelea kuimarisha ulinzi wa mipaka na Serikali inaagiza wageni wote wanaoingia nchini wafuate sheria za nchi na wale ambao hawatafuata sheria hizo watachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na wale wanaojihusisha na usafirishaji na wale wanaowaficha wahamiaji haramu kuacha tabia hizo kwa sababu Serikali itachukua hatua kali punde itakapojiridhisha kwamba kuna watu wamefanya vitendo hivyo.