Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 29 2017-09-06

Name

Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NAPE M. NNAUYE (K.n.y MHE. PROF. NORMAN A. S. KING) aliuliza:-
Pamoja na juhudi nzuri zinazofanywa na Serikali kupeleka umeme vijijini:-
Je, ni lini Vijiji 86 vya Wilaya ya Makete hususani Tarafa ya Ukwama, Lupalilo, Ikuwa, Matamba na Bulogwa watapatiwa umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Norman Adamson Sigalla King, Mbunge wa Makete, lililoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Nape Moses Nnauye, Mbunge wa Mtama, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini kupitia REA awamu ya tatu iliyoanza mwezi Machi, 2017. Utekelezaji wa mradi huu utakamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya mradi huu itajumuisha kufikisha umeme katika vijiji vyote vilivyobaki, vitongoji vyote, Taasisi zote za umma na maeneo ya pembezoni. Vijiji 28 kati ya vijiji 86 vya Wilaya ya Makete vilipatiwa umeme kupitia mradi wa REA II uliokamilika mwezi Desemba, 2016. Vijiji 58 na vitongoji vyake ikiwa ni pamoja na Bulongwa, Lupalilo, Matamba, Ikuwa na Ukwama vitapelekewa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu ulioanza mwezi Juni, mwaka huu ambao pia utakamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 29 vilivyobaki, itajumuisha kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 47.5, ufungaji wa transfoma 18, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 1,439. Mradi huu utakamilika mwezi Machi, 2019 na utagharimu shilingi bilioni 4.54.