Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2017-09-06

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER aliuliza:-
Mheshimiwa Rais alipokuwa anaomba ridhaa ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanzania mwaka 2015 aliahidi kuwa Serikali itakarabati mabwawa matatu ya josho, mto Mbu na Olkuro:-
(a) Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa Esilalei waweze kupata maji kwa ajili ya mifugo yao?
(b) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi wa Sepeko na Lepurko maji safi na salama?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS- TAMISEMI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Julius K. Laizer, Mbunge wa Monduli, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2016/2017, imekamilisha usanifu kwa ajili ya ukarabati wa mabwawa ya Joshoni na Olkuro na kubaini kuwa shilingi bilioni 1.45 zinahitajika kwa kazi hiyo. Mahitaji hayo yatazingatiwa katika mpango wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea
na utekelezaji wa miradi ya maji katika Vijiji vya Lendikinya Kata ya Sepeko ambao unatekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 868.07. Kazi imefikia asilimia 35 na itakamilika mwezi Octoba, 2017 kwa kuzingatia mkataba. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imeidhinisha shilingi milioni 639.5 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Nanja ambacho kipo Kata ya Lepurko ambao utahudumia pia shule ya Sekondari ya Nanja, Kata ya Sepeko.