Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 08 2017-09-05

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:-
Wilaya ya Kigamboni ina uwekezaji mkubwa katika sekta ya nyumba na viwanda, mahitaji ya umeme kwa sasa ni zaidi MW 20; lakini ni MW 8 tu zinazopatikana, nao umekuwa ukikatika mara kwa mara kutokana na mahitaji makubwa pamoja na uchakavu wa miundombinu ya umeme.
(a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha Kigamboni inapatikana umeme wa uhakika?
(b) Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha kupoozea umeme (substation) katika Wilaya ya Kigamboni kutokana na mahitaji makubwa ya umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) inakamilisha utekelezaji wa mradi wa uboreshaji umeme katika Jiji la Dar es Salaam kupitia mradi wa TEDAP. Mradi huu unahusisha ujenzi wa vituo vya kupooza umeme vya Mbagala na Kurasini. Kazi ya vituo hivyo ni pamoja na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya Kigamboni kwa kuwa Kigamboni sasa itakuwa ikipata umeme kutoka katika vituo hivi vya Mbagala na Kurasini badala ya Kipawa na Ilala kama ilipokuwa hapo nyuma. Ujenzi wa mradi huu ulianza mwaka 2012 na utakamilika mwishoni mwa mwezi Septemba, 2017.
(b) Mheshimiwa Spika, ili kulipatia ufubuzi wa kudumu tatizo la upatikanaji wa umeme eneo la Kigamboni, Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) linajenga njia ya kusafirisha umeme msongo wa kilovoti 132 kutoka Kurasini kwenda Dege – Kigamboni na kujenga kituo cha kupooza umeme chenye uwezo wa kilovoti 132 chenye uwezo wa kufua umeme wa MVA 120 sawa na MW 100. Taratibu za ujenzi zimeanza mwezi Agosti, 2017 na kazi inatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2018. Gharama ya mradi huu inakadiriwa kufikia shilingi bilioni tano.