Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 01 2017-09-05

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI E. KINGU aliluliza:-
Wilaya ya Ikungi hasa Jimbo la Singida Magharibi inakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa vituo vya afya na zahanati. Aidha, umbali mrefu wa kutafuta matibabu umekuwa ukisababisha adha na taabu kwa wananchi wa kata za Lyandu, Igelansomi na vijiji vya Mduguya, Kaangeni, Chengu na Mayahu.
Je, Serikali ipo tayari kushirikiana na wananchi katika kukamilisha ujenzi wa zahanati mpya na vituo vya afya vilivyoanzishwa kwa ushirikiano wa wananchi na Mbunge?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Emmanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza miradi ya vituo vya kutolea huduma za afya kwa kushirikisha nguvu za wananchi kupitia mpango wa fursa na vikwazo yaani O & OD. Serikali inampongeza Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi na wananchi wake kwa kuanza ujenzi wa vituo vya afya na zahanati.
Mheshimiwa Spika, katika kuunga mkono juhudi hizo, Serikali imetoa ruzuku ya maendeleo kwa Halmashauri hiyo, kiasi cha shilingi milioni 110 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya na zahanati katika Wilaya ya Ikungi. Aidha, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imetenga shilingi bilioni 1.49 kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa maboma yaliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi.