Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 3 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 29 2016-04-21

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:-
Mkoa wa Kigoma unaongoza kwa kuwa na vijana wengi wanamichezo na wasanii mfano Shaaban Robert, Diamond, Ali Kiba, Banana Zoro, Linex, Mrisho Mpoto na kadhalika:-
(a) Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika Mkoa wa Kigoma kwa kujenga Jumba la Sanaa (Theater Centre) ili vijana wa aina hii wawe na sehemu nzuri ya kuendesha shughuli zao?
(b) Kama Serikali inakubaliana na hoja hiyo, kituo hicho kitaanza kujengwa lini?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, WASANII NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Nicodemus Nsanzugwanko, Mbunge wa Kasulu Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatambua mchango mkubwa wa wasanii mashuhuri wenye asili ya Mkoa wa Kigoma kama vile Diamond, Ali Kiba, Banana Zoro, Mrisho Mpoto japokuwa nimepata taarifa kwamba huyu Mrisho Mpoto origin yake ni Mkoa wa Ruvuma na wengine ambao wameiletea sifa na kuitambulisha nchi yetu katika fani ya muziki na sanaa.
Mheshimiwa Spika, katika Sera ya Utamaduni ya mwaka 1999, Sura ya 4, kipengele Na.4.1.9 inasema, Serikali itahakikisha kuwa panakuwa na jengo la kisasa la sanaa za maonesho katika ngazi ya Taifa. Aidha, wananchi watahamasishwa kuhakikisha kwamba wanatenga maeneo ya maonesho.
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inaendelea kuhimiza Halmashauri na Manispaa zote nchini kutenga maeneo ya kujenga vivutio vya sanaa. Kuhusu Mkoa wa Kigoma, tunashauri Serikali ya Mkoa kwa kushirikisha Halmashauri zote za Mkoa huo ione umuhimu na namna bora ya kupanga na kutekeleza ujenzi wa Jumba la Sanaa. Aidha, tunatoa wito kwa Halmashauri zote nchini zione umuhimu wa kujenga majengo hayo.
(b) Mheshimiwa Spika, kazi ya kujenga miundombinu katika Halmashauri mbalimbali nchini ni jukumu la Halmashauri husika. Hivyo kila Halmashauri inashauriwa kutenga fedha katika bajeti zao kwa ajili ya Maendeleo ya Sanaa.