Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 31 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 246 2017-05-22

Name

Mohamed Juma Khatib

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chonga

Primary Question

MHE. MOHAMMED JUMA KHATIB aliuliza:-
Kumezuka wimbi kubwa sana lenye kutisha la ajali za bodaboda nchini kiasi cha kufanya hospitali zetu kupungukiwa na uwezo wa kuwahudumia waathirika wote wa ajali hizo.
(a) Je, Serikali inaweza kulieleza Taifa sababu za kutokea kwa wingi kwa ajali hizo?
(b) Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na utitiri wa ajali hizo bila kuathiri ajira hiyo ya bodaboda?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Mohammed Juma Khatib, Mbunge wa Chonga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, pikipiki za matairi mawili (Bodaboda) na za matatu (Bajaj) zilianza kutumika kubeba abiria mwaka 2008 Tanzania Bara na mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liliridhia vyombo hivyo vitumike kutoa huduma ya usafirishaji wa abiria. Sababu kubwa za kutokea kwa ajali zinazohusisha bodaboda na bajaj ni uzembe wa baadhi ya waendesha pikipiki na bajaji kutokufuata Sheria na Kanuni za Usalama Barabarani kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimekuwa nikijibu hapa Bungeni, Serikali inatambua biashara hiyo inayofanywa na pikipiki za kubeba abiria na inathamini mchango huo katika kutoa ajira katika mikoa yote ya Tanzania Bara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na ajali nyingi zinazosababishwa na bodaboda, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikichukua hatua dhidi ya waendesha pikipiki ambao hawazingatii Sheria ya Usalama Barabarani na kanuni zake pamoja na masharti ya leseni za usafirishaji. Aidha, Jeshi la Polisi limekuwa likitoa mafunzo kwa waendesha bodaboda juu ya matumizi bora ya barabara.