Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 59 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 495 2017-07-04

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMANI HIJA aliuliza:-
Kumekuwa na matukio yasiyo ya kawaida na kukaribia kuhatarisha amani katika Kisiwa cha Tumbatu:-
Je, Serikali haioni ipo haja ya kujenga Kituo cha Polisi katika Kisiwa hicho ili kukabiliana na matukio ya kiuhalifu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO NA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli yako matukio ya kihalifu yanayoripotiwa kutoka katika Kisiwa cha Tumbatu na Jeshi la Polisi linafanya jitihada ya kukabiliana na wahalifu kwa kutoa huduma za ulinzi na usalama katika kisiwa hicho kwa kufanya doria kila siku. Pamoja na doria, kumeanzishwa utaratibu wa detach ambapo askari wanakwenda kulinda kisiwa hicho na kubadilishana kwa zamu ili kuimarisha ulinzi. Aidha, ipo boti yenye uwezo wa kubeba Askari kumi. Iwapo uwezo wa kifedha ukiongezeka tutajitahidi kupata boti kubwa ya mwendo kasi na yenye uwezo wa kubeba Askari zaidi ya kumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaona haja ya kuwepo Kituo cha Polisi katika Kisiwa cha Tumbatu ili kusogeza huduma za ulinzi na usalama kwa kuzingatia jiografia ya kisiwa hicho na matukio ya uhalifu. Katika kutekeleza hilo, tayari Serikali imepata kiwanja chenye ukubwa wa mita za mraba 600 na makisio ya ujenzi wa kituo hicho umekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Bunge lako Tukufu naomba kutumia fursa hii kuhamasisha wadau na wananchi akiwemo Mheshimiwa Mbunge kushirikiana kuanza ujenzi wa kituo hiki wakati Serikali inakamilisha mipango yake ya kupata fedha.