Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 25 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 204 2017-05-15

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:-
Matumizi ya SHISHA yamegundulika kuwa ni miongoni mwa aina ya uvutaji wa sigara ambao wauzaji wengine huchanganya na aina mbalimbali za dawa za kulevya na vileo vikali na kusababisha vijana wadogo kuathiriwa kwa kiasi kikubwa.
Je, kwa nini Serikali hadi sasa inaendelea kuruhusu matumizi ya SHISHA kwenye baadhi ya migahawa na hoteli kubwa ambayo inatumiwa na watu wa rika zote?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Najma Giga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali mara baada ya kuona kuwa matumizi ya shisha yanaleta athari kubwa kwa afya za binadamu, kutokana na utafiti uliofanywa na Wizara ya Afya, Serikali ina mpango mkakati wa kutengeneza utaratibu wa kudhibiti na kutungia sheria kupiga marufuku utumiaji, uuzwaji na usafirishwaji wa shisha nchini Tanzania ili kuweza kuokoa afya za Watanzania walio wengi ambao ni nguvu kazi ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tukiwa tunasubiri kutungwa kwa sheria na kanuni, Mheshimiwa Waziri Mkuu alishaelekeza kupiga marufuku matumizi ya shisha na utekelezaji ulishaanza kutekelezwa mikoani ikiwemo Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na mikoa mingine.