Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 25 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 203 2017-05-15

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:-
Serikali inafanya zoezi la kimya kimya la utafutaji wa mafuta na gesi katika Jimbo la Mlimba bila kutoa taarifa rasmi kwa wananchi juu ya zoezi hilo:-
Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya mchakato huo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, utafutaji wa mafuta na gesi asilia katika Kitalu cha Kilosa Kilombero unaofanywa na Kampuni ya Swala Energy ulianza mwezi Februari, 2012. Kampuni hiyo ilianza kufanya utafiti wa awali wa kijiolojia kwa ajili ya kutambua aina na sifa za miamba iliyopo na kutoa taarifa ya mitetemo (seismic data).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na tafiti hizo, kampuni ilionesha uwezekano wa kuwepo kwa mafuta na gesi asilia katika eneo hilo. Eneo lililoainishwa kwa ajili ya uchimbaji wa kisima hicho lipo katika Kijiji cha Ipera Asilia katika Hifadhi Tengefu ya Bonde la Kilombero. Uchimbaji unatarajiwa kuanza mwezi Septemba, mwaka 2017 baada ya utafiti kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Februari, 2017, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) ilianza kutoa elimu kuhusu utafiti wa mafuta na gesi asilia na fursa zitakazopatikana kwa wananchi wa Mlimba hasa katika maeneo yanayozunguka mradi huo. Elimu hiyo itahusu pia athari za mazingira na ushiriki wa wananchi katika miradi mbalimbali kwa manufaa ya wananchi pamoja na Taifa kwa ujumla.