Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 32 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 257 2017-05-23

Name

Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Primary Question

MHE. HAMAD SALIM MAALIM aliuliza:-
Miongoni mwa stahiki za askari polisi anapohamishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine ni nauli ya askari huyo na wategemezi wake pamoja na fedha za kusafirishia mizigo:-
Iwapo mwajiri atashindwa kumlipa askari huyo stahiki
zake zote hizo, je, askari huyo atapaswa kuhama kwa gharama zipi na kuripoti mkoa wake mpya aliopangiwa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamad Salim Maalim, Mbunge wa Kojani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi hutoa uhamisho kulingana na mahitaji pale Inspekta Jenerali wa Polisi anapoona kuna umuhimu wa kuongeza nguvu eneo fulani ambalo ni tete kwa wakati huo. Hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 59(5)(a) ya Kanuni za Jeshi la Polisi (PGO). Askari anayehamishwa atalipwa mafao yake kama ilivyoelekezwa katika Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma, Toleo Na. 259 iwapo hakuhamishwa kwa makosa ya kinidhamu. Aidha, askari anayeomba kuhama eneo moja kwenda eneo lingine kwa sababu zake binafsi hatalipwa mafao hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia maelezo hayo, inapotokea dharura ya askari kuhitajika kwenda kutoa huduma eneo lingine, askari husika atatekeleza amri ya uhamisho haraka wakati stahili zake zinafanyiwa kazi kwa mujibu wa taratibu za fedha. Kwa taratibu za Kijeshi, askari hawezi kusubiri malipo katika mazingira ambayo anakwenda kuokoa maisha ama kulinda maslahi ya Taifa katika eneo husika.