Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 22 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 189 2017-05-11

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-
Vijiji 48 vya Jimbo la Same Magharibi vyenye zaidi ya kaya 2,943 havijapatiwa umeme wa REA japokuwa vina mahitaji makubwa ya umeme.
Je, ni ipi ratiba ya kuwasambazia umeme wananchi hawa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi kabambe wa usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu umeanza nchi nzima tangu Machi, 2017. Mradi huu unajumuisha vipengele vya miradi vitatu vya Densification, Grid Extension pamoja na Off Grid Renewable.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zitakazofanyika ni kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji, vitongoji vyote, taasisi za umma na maeneo ya pembezoni ambayo hayajafikiwa na miundombinu ya umeme, ikiwa ni pamoja na visiwa.
Mradi wa REA Awamu ya Tatu utakamilika mwaka 2020/2021. Vijiji vya Jimbo la Same Magharibi vitapatiwa umeme kupitia mradi huu wa REA Awamu ya Tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo itahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 67.81. Ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 261, ufungaji wa transfoma 43 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja 2,457.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hii itagharimu shilingi bilioni 10.8.