Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 17 Energy and Minerals Wizara ya Madini 144 2017-05-04

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:-
Tagamenda Substation ni kituo kikubwa kati ya vituo vinavyosafirisha umeme wa Gridi ya Taifa kwani kinapokea umeme kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi, lakini vijiji vya Tagamenda, Ikuvilo na Wangama vinavyozunguka kituo hicho havina huduma ya umeme ingawa ndivyo vinalinda kituo hicho.
(a) Je, ni kwa nini Serikali inashindwa kutoa huduma
ya umeme katika vijiji vinavyozunguka kituo hicho?
(b) Je, ni sababu gani zinazofanya vijiji hivyo kukosa kupatiwa huduma hata ya umeme wa REA?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Kitongoji cha Malulumo
Kijiji cha Tegamenda kiliwekwa katika Mpango wa kupatiwa umeme kupitia Shirika la Umeme TANESCO katika mwaka 2015/2016. Kazi hiyo ilianza Mei, 2016 na inakamilika Juni, 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi za kupeleka umeme katika Kitongoji hicho zimejumuisha ujenzi wa njia ya msongo wa umeme wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa moja; ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 1.4; ufungaji wa transfoma moja pamoja na kuwaunganishia umeme wateja 70. Kazi hii imekamilika kwa asilimia 90 na inagharimu shilingi bilioni 93.1.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu umeanza nchi nzima tangu mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele-mradi vitatu vya densification, grid extension pamoja na off-grid renewable vinavyolenga kuongeza wigo wa umeme katika vijiji vyote nchini, vitongoji vyote vilivyobaki, taasisi za umma na maeneo ya pembezoni ambayo hayajafikiwa na miundombinu ya umeme ikiwa ni pamoja na visiwa. Vijiji vya Ivukilo, Wangama pamoja na maeneo mengine ya kijiji cha Tagamenda vimewekwa katika utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu wa Densification na Grid Extenson utakaokamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivi itajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 10.3; ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 9.7; ufungaji wa transfoma tatu pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 300. Gharama ya kazi hii ni shilingi bilioni 14.45.