Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 2 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 11 2016-04-20

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Serikali iliahidi kupeleka gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mgololo lakini hadi sasa gari hilo halijapelekwa:-
Je, ni lini gari hilo litapelekwa ili liweze kusaidia Vijiji vya Idete, Itika, Holo, Isaula, Rugema, Makungu, Rugolofu na Kitasengwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ina gari moja linalotumika kuhudumia wagonjwa. Hata hivyo, gari hilo ni chakavu kiasi cha kuhitaji matengenezo ya mara kwa mara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kila Halmashauri inapaswa kuweka kipaumbele na kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya kubebea wagonjwa kwa kuzingatia mahitaji yaliyopo. Katika bajeti ya mwaka 2016/2017, Halmashauri imeomba shilingi milioni 543.0 kwa ajili ya kununua magari matatu (ambulance) ambapo kati ya hayo gari moja litapelekwa katika Kituo cha Afya Mgololo na mengine katika Vituo vya Afya vya Sadani na Kasanga ili yasaidie kuwafikisha wagonjwa wenye dharura kwenye vituo vya kutolea huduma kwa haraka.