Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 7 | Sitting 11 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 92 | 2017-04-24 |
Name
Hassan Elias Masala
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nachingwea
Primary Question
MHE. HASSAN E. MASALA Aliuliza:-
Barabara ya Nanganga – Nachingwea – Masasi imeshafanyiwa upembuzi yakinifu toka mwaka wa 2015/2016.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MWASILIANO
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Elias Masala, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), ilikamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mwaka wa fedha wa 2014/2015 kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Masasi – Nachingwea hadi Nanganga. Aidha, katika mwaka wa 2017/2018 Wizara imeomba kutengewa shilingi bilioni 3.515 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved