Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 73 2017-04-19

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE Aliuliza:-
Waliokuwa wafanyakazi wa Hoteli ya Seventy Seven ya Arusha hawajalipwa mafao yao hadi sasa:-
Je ni lini watalipwa mafao yao?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, waliokuwa wafanyakazi wa Hoteli ya Seventy Seven - Arusha wapato 238 waliachishwa kazi mwaka 2000 na kulipwa mafao yao kwa mujibu wa taratibu na sheria. Katika zoezi la ulipaji wa mafao ya wafanyakazi hao, Serikali kupitia iliyokuwa PSRC ilitoa na kulipa kiasi cha shilingi 217,366,296 mwezi Januari, 2000 kama mafao ya wafanyakazi hao. Baada ya malipo hayo watumishi hao waliwasilisha malalamiko kuwa wamepunjwa. PSRC ilihakiki madai hayo na baada ya kujiridhisha mwezi Agosti, 2000 Serikali ilitoa idhini ya kulipa tena kiasi cha shilingili 273,816,703 kugharamia mapunjo ya mishahara na mafao ya wafanyakazi hao.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, wafanyakazi hao tayari walishalipwa mafao yao kwa mujibu wa sheria na taratibu na hawastahili kudai malipo yoyote ya nyongeza.